Home Soka Stars Yatua Sudan

Stars Yatua Sudan

by Sports Leo
0 comments

Timu ya taifa ya Tanzania (Taifa stars) imewasili mjini Khartoum nchini Sudan kuelekea mchezo wa kimataifa wa kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika kwa wachezaji wa ndani(Chan) ikitokea Kigali Rwanda ilipokwenda kucheza mchezo wa kirafiki.

Baada ya mchezo huo na The amavubi ambao uliisha kwa suluhu Stars ilipaa mpaka jijini Khartoumu kuwahi maandalizi ya mwisho katika mchezo huo wa marejeano ambapo mchezo wa awali uliofanyika jijini Dar es salaam uliisha kwa Stars kufungwa 1-0.

Ili ifuzu Stars inahitaji kufunga mabao kuanzia mawili huku isiruhusu kufungwa mabao mengi ili kuwa na tofauti ya mabao ya ugenini na nyumbani ili kupata nafasi hiyo ya kushiriki fainali hizo.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited