Home Soka Tariq Seif Arejea

Tariq Seif Arejea

by Sports Leo
0 comments

Staa wa klabu ya Yanga aliyekua anasumbuliwa na maumivu ya nyama za paja Tariq Seif Kiakala amerejea mazoezini kujiunga na wenzake kujiandaa na mzunguko wa pili wa ligi kuu Tanzania bara.

Straika huyo aliyeumia katika mechi dhidi ya Biashara united uwanja wa taifa tayari yupo fiti baada ya kufanya mazoezi kwa siku kadhaa na sasa ni suala la mwalimu Luc Eymael kumpanga tu.

“Nitakuwa tayari kuisaidia timu yangu mwalimu akinipa nafasi, naamini kadiri siku zinavyozidi kwenda mbele ndipo nitakapokuwa fiti zaidi,” alisema Tariq ambaye alijiunga na Yanga katika usajili wa dirisha dogo uliofungwa Januari 15, mwaka huu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited