Home Soka Waamuzi Sita Kuamua Yanga vs Simba

Waamuzi Sita Kuamua Yanga vs Simba

by Sports Leo
0 comments

Bodi ya ligi nchini TPLB imetangaza rasmi kuwa mchezo wa ligi kuu nchini baina ya Yanga sc dhidi ya Simba sc utachezeshwa na waamuzi sita ili kuleta ufanisi zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari katika uwanja wa Benjamini Mkapa katika mkutano maalumu na wanahabari mtendaji mkuu wa TPLB Almas Kazongo alisema kuwa wao kama wasimamizi wa mchezo huo wameona inafaa kutumia waamuzi sita ambapo wanne watakua kama ilivyo mechi zingine huku wale wawili watakaoongezeka watakua nyuma ya magoli.

Mchezo huo wa kusisimua unatarajiwa kufanyika Novemba 7 siku ya jumamosi katika uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar es salaam ambapo katika mchezo wa mwisho timu hizo kukutana Yanga alifungwa mabao 4-0.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited