Home Soka Wahispania Wamnyemelea Kagere

Wahispania Wamnyemelea Kagere

by Sports Leo
0 comments

Wakati ikidaiwa ameanza kuporomoka kiwango licha kuwa ndio anaongoza katika mbio za kuwania kiatu cha dhahabu,Meddie Kagere amewavutia wahispania ambao wanamuhitaji haraka nchini humo kujiunga na klabu yao.

Timu hiyo ambayo inashiriki ligi daraja la kwanza  inamuhitaji staa huyo ili kwenda kuongeza nguvu katika harakati za kupanda ligi kuu nchini humo(La liga).

Kagere aliyejinga na Simba sc akitokea nchini Kenya katika klabu ya Gormahia fc ameibuka kuwa mshambuliaji tegemeo klabuni hapo huku akifanikiwa kutwaa tuzo ya mfungaji bora msimu uliopita na tayari ameshafunga mabao 11 msimu akiwa kinara wa ufungaji.

banner

Meneja wa mchezaji huyo Patrick Gakumba tayari amethibitisha kuwasili kwa ofa ya mchezaji huyo huku akisubiria uamuzi wa klabu ya Simba kama itakua tayari kumuuza staa huyo ama kumtoa kwa mkopo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited