Home Soka Yanga Sc Yaipiga 5 Polisi Tanzania

Yanga Sc Yaipiga 5 Polisi Tanzania

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imeendelea kusimamisha mnara wa mabao matano baada ya kuibamiza Polisi Tanzania kwa mabao 5-0 katika mchezo wa kombe la shirikisho la Azam Sports hatua ya 32 bora uliofanyika katika uwanja wa Chamazi jijini Dar es salaam.

Ikianza mchezo bila mastaa wake Maxi Nzengeli,Djigui Diarra,Dickson Job,Ibrahim Hamad,Yao Kouassi,Pacome Zouzou ambao walikua jukwaani,Klabu hiyo ilianza kupata bao mapema dakika ya 13 kupitia kwa Joseph Guede kisha Farid Mussa dakika ya 33 akafunga bao la pili na dakika ya 45 Guede akafunga bao la tatu.

Clement Mzize ambaye aliingia kipindi cha pili alifunga bao la tatu dakika ya 82 kisha Shekhan Ibrahim akafunga bao la tano kwa penati dakika ya 87 baada ya Mzize kuangushwa katika eneo la 18.

banner

Kwa ushindi huo Yanga sc sasa imefuzu hatua ya 16 bora ya michuano hiyo ambapo sasa inasubiri mzunguko ukamilike kisha ianze mbio za kuitafuta robo fainali.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited