Home Soka Yanga Yaibamiza Mlandege

Yanga Yaibamiza Mlandege

by Dennis Msotwa
0 comments

Klabu ya Yanga sc imeibuka na ushindi wa mabao 2-0 mchezo wa kirafiki dhidi ya Mlandege Fc kutoka visiwani Zanzibar uliofanyika katika uwanja wa Chamazi Complex jijini Dar es salaam.

Yanga iliyochezesha vikosi viwili huku kile cha mastaa kikicheza dakika 45 za kipindi cha pili ilipata mabao yake kupitia kwa Waziri Junior kwa penati kipindi cha kwanza baada ya beki wa Mlandege kuunawa mpira ndani ya 18 wakati akijaribu kuokoa pasi ya Haruna Niyonzima.

Mukoko Tonombe aliipatia Yanga sc bao la pili dakika ya 59 kwa shuti kali baada ya kupokea pasi ya Yacouba Sogne na mpaka dakika ya 90 matokeo yalisalia hivyo hivyo.

banner

Yanga itasafiri kesho kuifuata Kagera Sugar siku ya Jumamosi mchezo utakaofanyika katika uwanja wa Kaitaba mkoani humo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited