Home Soka Yanga Yatinga Nusu Fainali

Yanga Yatinga Nusu Fainali

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc  imefanikiwa kufuzu hatua ya nusu fainali ya michuano ya kombe la Shirikisho la Azam baada ya kuifunga timu ya Kagera Sugar kwa mabao 2-1 mchezo uliofanyika katika uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam.

Kagera walikua wa kwanza kupata bao dakika ya 19 kupitia kwa Awesu Awesu huku Yanga wakisawazisha dakika ya 51 kupitia kwa David Molinga na dakika ya 71 Mrisho Ngassa alifanyiwa madhambi nje kidogo ya mstari wa 18 lakini mwamuzi aliamuru iwe penati na Deus Kaseke akaifungia goli la pili.

Awese Awese alionyeshwa kadi nyekundu na kuwafanya Kagera kumaliza mchezo wakiwa pungufu japo walimiliki mchezo mpaka filimbi ya Mwisho.

banner

Yanga itawalazimu kusubiri mpambano kati ya Simba sc dhidi ya Azam fc ili kujua watakayekutana nae kuelekea hatua ya fainali.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited