Home Makala Yondani Anukia Kagera Sugar

Yondani Anukia Kagera Sugar

by Sports Leo
0 comments

Mchezaji wa zamani wa klabu ya Yanga sc Kelvin Yondani yupo njiani kujiunga na klabu ya Kagera Sugar akitokea klabu ya Geita Gold Fc ambapo amedumu kwa takribani nusu msimu pekee alipojiunga akitokea Polisi Tanzania.

Yondani yupo kwenye mazungumzo ya kuvunja mkataba wake na Geita Gold Fc ili akamilishe usajili huo wa kujiunga na Kagera Sugar ambayo imekua na matatizo kadhaa katika safu ya ulinzi ambayo imekua ikilegalega mara kadhaa.

Yondani ni beki mzoefu nchini ambapo alifanikiwa kuichezea klabu ya Yanga sc na timu ya Taifa kwa muda mrefu akiwa kama nahodha pia hivyo uzoefu huo utaenda kuisaidia Kagera Sugar Fc kuimarisha eneo la ulinzi.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited