Home Soka Katwila Aitisha Yanga sc

Katwila Aitisha Yanga sc

by Sports Leo
0 comments

Kocha Zubeiry Katwila ameipa vitisho klabu ya Yanga sc kuwa yuko tayari kupambana katika mchezo wa ligi kuu utakaofanyika siku ya Jumamosi katika uwanja wa Azam Complex uliopo Chamazi jijini Dar es salaam.

Katwila ambaye ni kocha wa zamani wa Ihefu Sc ambapo amewahi kuifunga Yanga sc alipokua kocha wa klabu hiyo mchezo uliochezwa mkoani Mbeya katika uwanja wa Highlanders Estate kwa mabao 2-1 na kuipa kipigo cha kwanza cha ligi kuu msimu huu.

Kuelekea mchezo huo Katwila amesema kuwa ataingia katika mchezo huo kwa lengo la kupambana ili kupata alama tatu.

banner

“Tutaingia kwa kuwaheshimu Yanga Jumamosi na siyo kuwaogopa tunacheza na timu yenye wachezaji 11 kama sisi na changamoto tunayoipitia ni kipindi cha mpito timu nyingi huwa zinapitia nyakati ngumu kama hizi matokeo haya hayanifurahishi, nimeandaa programu nyingine za mazoezi na kuwapa wachezaji muda zaidi wa mazoezi wa kuongeza viwango vyao.”Alisema Katwila

Mtibwa Sugar ipo katika hatari ya kushuka daraja kutokana na kuwa na kiwango kisichoridhisha huku ikiwa katika nafasi ya mwisho ya msimamo wa ligi kuu ikiwa na alama tano pekee katika michezo kumi na mbili ya ligi kuu ya Nbc.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited