Home Soka Yanga Sc Yashusha Mashine ya Magoli

Yanga Sc Yashusha Mashine ya Magoli

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Yanga sc imemtambulisha mshambuliaji Joseph Guede kama usajili wake wa mwisho wa dirisha dogo la usajili msimu huu akiwa kama mchezaji huru baada ya mchezaji huyo kumalizana na klabu ya Tulazpur ya nchini Uturuki.

Mshambuliaji huyo raia wa Ivory Coast amejiunga na Yanga sc kwa mkataba wa miaka miwili akichukua nafasi ya Hafiz Nkokoni ambaye kocha Miguel Gamondi amesisitiza kuwa haingii katika mfumo wake wa uchezaji na kuhitaji aletewe mshambuliaji mwingine.

Katika kipindi chake cha soka mchezaji huyo amewahi kuhudumu klabu za As Far Rabat ya nchini Morroco,Emirate Club ya Uarabuni na Tulazpur ya nchini Uturuki ambayo aliachana nayo tangu mwezi Septemba mwaka jana.

banner

Yanga sc sasa itakua na washambuliaji watatu wa katika wakiwemo Kennedy Musonda na Clement Mzize ambao watakua na kazi ya kufunga mabao ili kushinda makombe jangwani.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited