Home Soka Benchika Asema Mazito kwa Wanasimba Sc

Benchika Asema Mazito kwa Wanasimba Sc

by Sports Leo
0 comments

Kocha Mkuu wa Simba SC, Abdelhak Benchikha amesema kuwa anapambana kwa moyo wake wote ili kuhakikisha timu hiyo inachukua ubingwa wa Ligi kuu Tanzania Bara pamoja na kufika mbali kwenye Ligi ya Mabingwa barani Afrika.

“Nimekuja Tanzania kushinda mataji na nimeridhishwa na usajili ambao tumefanya hivyo Simba ya kesho ni nzuri,”Alisema kocha huyo mwenye rekodi ya kutwaa taji la kombe la shirikisho barani Afrika baada ya kuifunga Yanga sc.

Benchika tangu atue Simba sc ameonyesha msisitizo hasa katika suala la nidhamu ambapo amewasimamisha wachezaji Cletous Chama na Nassoro Kapama ambaye tayari ameondoshwa kwa mkopo kikosini humo huku akisajili majembe ya kazi kurudisha furaha kwa mashabiki wa Simba sc.

banner

Usajili wa Omar Pa Jobe,Fredy Michael,Edwin Balua,Babacar Sarr unatajwa kuwa ni moja ya mapendekezo ya kocha huyo ili kuja kuleta ushindani wa kutosha katika ligi kuu nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited