Home Makala Guede Kuwakosa Kmc

Guede Kuwakosa Kmc

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa klabu ya Singida Black Stars Joseph Guede anatarajiwa kuukosa mchezo wa ligi kuu ya Nbc baina ya timu hiyo na Kmc utakaofanyika Septemba 12 katika uwanja wa Ccm Liti mjini Singida.

Guede ataungana na mastaa kama Jimson Mwinuke ambaye naye ana majeraha huku mastaa wengine kama Mohammed Camara na Maurouf Tchakei nao wataikosa mechi hiyo kutokana na kuchelewa kuripoti kutoka timu zao za Taifa.

Guede mshambuliaji wa zamani wa klabu ya Yanga sc amejiunga na timu hiyo yenye makao yake makuu mkoani Singida baada ya kumaliza mkataba wake wa miezi sita Jangwani.

banner

Singida Black Stars na Kmc zinatarajiwa kuwa na mchezo wenye upinzani mkali kutokana na vikosi hivyo kuwa na wachezaji mahiri sambamba na uchumi ulioimara tofauti na vilabu vingine ukiwatoa Simba sc,Azam Fc na Yanga sc.

Kocha Patrick Aussems na msaidizi wake Dennis Kitambi wana kazi kubwa ya kuhakikisha ushindi unapatikana kwa timu hiyo yenye alama sita ikicheza michezo miwili ya ligi kuu ya Nbc nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited