Home Soka Yanga sc Yawasili Arusha

Yanga sc Yawasili Arusha

by Sports Leo
0 comments

Msafara wa mastaa wa klabu ya Yanga sc umefanikiwa kuwasili salama jijini Arusha kwa ajili ya mchezo wa ligi kuu ya Nbc nchini dhidi ya Coastal Union unatarajiwa kufanyika katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta jijini humo.

Yanga sc imewasili ikiwa na zaidi ya asilimia kubwa ya mastaa wake ambao wameonekana uwanja wa ndege wakiwasili kwa ajili ya mchezo huo huku kipa Djigui Diarra akikosekana katika msafara huo huku haijajulikana sababu kuu ya kukosekana huko.

Yanga sc itakua na kibarua kigumu kuchukua alama tatu mbele ya Coastal Union ambayo wiki hii imemtambulisha kocha Juma Mwambusi kama kocha mkuu klabuni hapo.

banner

Ikiwa inawania ubingwa wa ligi kuu nchini Yanga sc mpaka sasa imeshinda michezo yote sita iliyocheza ya ligi kuu ikisusanya alama 18 huku Coastal Union ikiwa na alama nane baada ya kucheza michezo nane ya ligi kuu ya Nbc nchini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited