Shirikisho la soka nchini Tff limemwalika Rais wa shirikisho la soka barani Afrika Caf Ahmed Ahmed kuwa mgeni rasmi wa mechi baina ya watani wa jadi Simba na Yanga itakayofanyika jumapili.
Barua iliyotumwa na Tff kwenda Yanga ambao ni wenyeji wa mchezo huo imethibitisha kuwa Rais huyo atahudhuria mchezo huo kama mgeni rasmi wa mchezo huo mkubwa barani Afrika.
Rais huyo huyo atawasili nchini Jumamosi na ataondoka siku ya jumanne ambapo licha kuhudhuria mechi hiyo pia atazungumza na viongozi wa serikali.