Home Soka Simba Sc Waituliza Kagera Sugar

Simba Sc Waituliza Kagera Sugar

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imefanikiwa kupunguza pengo la alama kati yake na Vinara wa ligi kuu nchini Yanga sc baada ya jana kuifunga klabu ya Kagera Sugar kwa mabao 2-0 katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es salaam.

John Bocco alifanikiwa kufunga kwa penati dakika ya 42 baada ya Hassan Dilunga kuangushwa katika eneo la 18 na David Luhende na mpaka timu zinaingia mapumziko matokeo yalibaki hivyo hivyo.

Dakika ya 48 kipindi cha pili dakika ya 48 Said Ndemla aliipatia Simba sc bao la pili baada ya kufanya shambulizi la ghafla ambapo Cletous Chama alimpasia mfungaji ambaye aliukwamisha mpira nyavuni.

banner

Simba sc sasa imepanda mpaka nafasi ya tatu ikiwa na alama 19 huku Yanga akiwa kinara kwa alama 23 ambapo timu hizo zitakutana siku ya jumamosi Novemba 7 katika uwanja wa Mkapa jijini Dar es salaam.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited