Home Soka Mo Atuliza Hali ya Hewa

Mo Atuliza Hali ya Hewa

by Sports Leo
0 comments

Muwekezaji wa klabu ya Simba sc Mohamed Dewji ni kama ametuliza hali ya hewa baada ya kuthibitisha kuwa Staa Cletous Chama ameongeza mkataba wa miaka miwili kuendelea kusalia katika klabu hiyo mpaka mwaka 2022.

Mo dewji alisema hayo baada ya kuwa na kelele za muda kutoka kwa watani wa jadi ambao walijinasibu kumsainisha kiungo huyo mwenyeji wa ndola nchini Zambia.

Pia tajiri huyo namba moja nchini kwa mujibu wa jarida la Forbes amethibitisha kuhusu timu hiyo kutomhitaji kiungo Mukoko Tonombe wa Yanga sc huku kwa maana bado suala la mchezaji huyo halijafika katika kamati ya usajili ya timu hiyo hivyo ni propaganda tu.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited