Home Makala 1.5B Kumng’oa Ahou Msimbazi

1.5B Kumng’oa Ahou Msimbazi

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba Sc imesisitiza kuwa haiko tayari kumuachia kiungo mshambuliaji Jean Charles Ahoua kwa dau chini ya shilingi bilioni 1.5 za kitanzania.

Awali klabu hiyo iliwasiliana na Kaizer Chiefs kuwa haitamuuza kiungo mshambuliaji Jean Charles Ahoua (23) kutokana na kocha Fadlu Davis kuwa katika mipango yake ya msimu ujao.

Hata hivyo sasa hivi mabosi wa timu hiyo wapo tayari kurudi mezani ikiwa anayemuhitaji Jean Ahoua aweke USD 600K (Tshs 1.5 Bilioni) ili kumuachia mchezaji huyo ambapo itakua na uhakika wa kupata kiungo mwingine sokoni.

banner

Kaizer Chiefs inavutiwa na inamfatilia kiungo mshambuliaji Jean Charles Ahoua ambaye amekuwa na msimu bora sana akiwa na klabu hiyo akiongoza katika safu ya wafungaji bora mpaka sasa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited