Home Makala Aucho Mbioni Kuivaa Simba sc

Aucho Mbioni Kuivaa Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Kiungo Khalid Aucho ambaye alikua na majeruhi kwa wiki kadhaa tayari amerejea kikosini Yanga sc ambapo ameonekana akifanya mazoezi na wenzake baada ya kumaliza programu ya utimamu wa mwili.

Kiungo huyo kipenzi cha mashabiki wa klabu ya Yanga sc aliumia  katika mchezo dhidi ya Mtibwa Sugar jeraha ambalo lilipona lakini alijitonesha katika mazoezi ya timu ya Taifa ya Uganda alikoitwa wiki chache zilizopita katika michezo ya kimataifa.

Aucho anakuja kuongeza ubora wa safu ya kiungo ya Yanga sc ambayo ilipwaya kutokana na kuumia kwake pamoja na kiungo Feisal Salum hivyo kufanya kikosi kuwa na viungo wa asili wa eneo la kati wawili pekee ambao ni Zawadi Mauya na Salum Abubakari ‘Sure Boy’.

banner

Kocha Nabi sasa atakua anafurahia kurejea kwa Aucho kutokana na michezo migumu iliyo mbele yake dhidi ya Namungo Fc na Simba sc ambayo itapisha wiki pekee huku michezo hiyo ikibeba picha halisi ya safari ya ubingwa ya klabu hiyo ambao iliukosa kwa takribani miaka minne mfululizo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited