Home Makala Makazi Mapya Ya Yanga 2020/2021

Makazi Mapya Ya Yanga 2020/2021

by Sports Leo
0 comments

Bilionea wa GSM ,Ghalib Mohhamed amewahamisha wachezaji wa Yanga pamoja na benchi la ufundi ili kupata utulivu kwenye makazi yao mapya yaliopo Kigamboni kwa ajili ya maandalizi ya msimu ujao wa ligi kuu bara unaoanza Septemba 6,2020.

Yanga imewekwa kwenye majengo maarufu ya Avic yaliyojitenga na yenye utulivu mkubwa huku ndani yake pakiwemo vifaa vyote vya michezo pamoja na uwanja wa kufanyia mazoezi kwa timu.

Tajiri huyo ameamua kuwaficha huko Yanga Sc ili kuwa kambi yao maalumu na kutofikiria tena suala la hotelini isipokuwa mchezaji atakayejisikia kufanya mazoezi mda wowote awe huru kwani hiyo ndio kambi yao kwa sasa na hakuna mtu yeyote anayewezakuingia pasipo ruhusa au taarifa zake kamili

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited