Home Makala Mbuna Akimbilia Tanzania Prisons

Mbuna Akimbilia Tanzania Prisons

by Sports Leo
0 comments

Mchezaji wa zamani wa Yanga Sc na Majimaji FC Fred Mbuna, amejiunga na Tanzania Prisons kama kocha msaidizi wa timu hiyo ambayo Disemba 28, 2024 ilitangaza kuvunja mkataba wa aliyekuwa kocha wao mkuu Mbwana Makata.

Mbuna kabla ya kujiunga na Tanzania Prisons alikuwa Kocha Msaidizi wa timu ya Yanga Princess akisaidiana na kocha Edna Lema.

Kocha huyo anaenda kuungana kocha Amon Jossiah ambaye amechukua nafasi hiyo kikosini akichukua nafasi ya Mbwana Makata ambaye alitimuliwa kutokana na matokeo mabaya.

banner

Katika msimamo wa ligi kuu nchini mpaka sasa Tanzania Prisons imecheza michezo 16 ikiwa na alama 14 katika nafasi ya 13 ya msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini.

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited