Home Makala Mkude Aondoka Simba sc

Mkude Aondoka Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Baada ya kudumu katika kikosi cha Simba sc kwa takribani miaka 13 tangu asajiliwe rasmi katika timu ya wakubwa ya klabu hiyo akitokea Simba sc hatimaye kiungo wa klabu hiyo Jonas Mkude rasmi anaondoka klabuni hapo baada ya mkataba wake kuisha.

Simba sc wameafikiana kuachana na mchezaji huyo kutokana na mapendekezo ya benchi la ufundi katika kuboresha timu hiyo ambapo wametaka watafutiwe kiungo mwingine kuongeza nguvu kuungana na Mzamiru Yassin na Sadio Kanoute.

Tayari timu za Singida Fountain Gate Fc imeonyesha nia ya kumchukua staa huyo kuziba nafasi ya Yusuph Kagoma ambaye yupo mbioni kujiunga na Yanga sc.

banner

Mpaka sasa Simba sc tayari imeachana na mastaa kadhaa kama vile Gadiel Michael,Victor Akpan,Mohamed Outtara,Erasto Nyoni,Beno Kakolanya,Nelson Okwa huku pia ikisafisha baadhi ya watu wa benchi la ufundi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited