Home Makala Mturo Apewa Fainali FA

Mturo Apewa Fainali FA

by Sports Leo
0 comments

Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) limetangaza majina sita ya waamuzi watakaochezesha mchezo wa fainali kombe la Azam (ASFC) utakaofanyika Jumapili August 2,2020 mkoani Sumbawanga Uwanja wa Nelson Mandela kati ya Simba Sc na Namungo Fc.

Abubakari Mturo kutoka Mtwara ni moja ya muamuzi atakayekuwepo katika mchezo huo baada ya kutoka kwenye kifungo cha miezi mitatu tangu Februari baada ya kushindwa kumudu mchezo kati ya Yanga Sc dhidi ya Lipuli Fc.

Waamuzi wengine wakiwa ni Abdallah Mwinyimkuu kutoka Singida,Ahmed Arajiga kutoka Manyara,Ramadhani kayoko kutoka Dar-es-salaam,Abdullaziz Ally kutoka Arusha na Hamdan Said kutoka Mtwara.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited