Home Makala Simba sc Kucheza za Kimataifa

Simba sc Kucheza za Kimataifa

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc itashiriki katika michezo kadhaa ya kirafiki ya kimataifa kwa ajili ya kujiandaa kikamilifu na ligi kuu pamoja na michuano ya klabu bingwa barani Afrika itakayoanza mapema mwezi ujao.

Simba sc imetoa ratiba fupi ya michezo mbalimbali ya kimataifa ambayo itashiriki katika kipindi hiki cha mapumziko ya ligi kuu nchini kupisha michuano ya kimataifa ya kufuzu mashindano mbalimbali ambapo baadhi ya nyota wa klabu hiyo wamejiunga na kambi za timu zao za Taifa.

Katika ratiba fupi iliyotolewa na klabu hiyo inaonyesha kwamba itakua na mchezo wa kwanza August 28 dhidi ya Asante Katoko utakaochezwa nchini Sudan huku siku tatu baadae itacheza na Al Hilal hukohuko Sudan kisha watarejea nchini kucheza na timu ya AS Arta Solar ya Djibout mchezo ambao utafanyika nchini Tanzania.

banner

Lengo kubwa la michezo hiyo ni kuiandaa timu kushiriki michuano mbalimbali ya ndani na nje ya nchi.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited