Home Makala Simba Sc Yashinda 1-0 Dhidi ya Kagera Sugar

Simba Sc Yashinda 1-0 Dhidi ya Kagera Sugar

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba Sc imefanikiwa kuibuka na ushindi kiduchu wa bao 1-0 dhidi ya Kagera Sugar katika mchezo wa ligi kuu ya Nbc nchini uliofanyika katika uwanja wa Kmc Complex mwenge jijini Dar es Salaam.

Bao pekee la Steven Mukwala dakika ya 17 ya mchezo liliwahakikishia Simba Sc alama tatu katika mchezo huo na kufikisha alama 77 katika nafasi ya pili ya msimamo wa ligi kuu ya Nbc nchini.

Kagera Sugar hawakuwa na cha kupoteza katika mchezo huo kutokana na kuwa wameshashuka daraja na msimu ujao watashiriki ligi daraja la kwanza.

banner

Simba sc ilitumia wachezaji wengi ambao hawaanzi mara kwa mara katika kikosi cha kwanza ili kutunza nguvu kwa ajili ya mchezo wa jumatano dhidi ya Yanga sc ambao Simba sc wanapaswa kushinda ili kutwaa ubingwa wa ligi kuu ambao wana takribani miaka mitatu hawajachukua.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited