Home Makala Sven Akubali Uwezo Wa Miqussone

Sven Akubali Uwezo Wa Miqussone

by Sports Leo
0 comments

Kocha mkuu Simba Sc, Sven Vandenbroeck ameweka wazi kuwa kwa sasa anahitaji viungo wakali wenye uwezo kama Luis Miqussone ambao anaamini watampa matokeo ndani ya uwanja.

Miqusssone ambaye ni kiungo wa Simba Kabla ya Ligi kuu bara kusimamishwa ili kupambana na maambukizi ya virusi vya Corona alianza kuingia kwenye mfumo wa Sven kutokana na kubadili matokeo akiwa ndani ya uwanja licha ya kutumia dakika chache.

Mbelgiji huyo ametoa mapendekezo yake ya aina ya wachezaji anaowataka huku akisisitiza anahitaji viungo wenye uwezo wa kunyumbulika zaidi kama ilivyo kwa Miqussone.

banner

Akiwa ni mchezaji aliyejiunga na Simba kwenye usajili wa dirisha dogo msimu huu Januari ,Miqussone alicheza mechi nane na kufunga mabao matatu na kutoa pasi moja ya bao lililofungwa na Meddie Kagere kwenye mchezo dhidi ya Biashara United.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited