Home Soka Yanga Sc Ubabe Ubabe

Yanga Sc Ubabe Ubabe

by Sports Leo
0 comments

Yanga sc imeendeleza Ubabe kwa Simba sc baada ya kuifunga 1-0 na kufanikiwa kuingia Fainali ya kombe la Ngao ya jamii katika mchezo uliofanyika katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

Simba sc licha ya kuwa na kikosi kisichokua na muunganiko iliamua kupishana na Yanga sc dakika zote tisini za mchezo huo uliokua na kasi ya kutosha huku kukiwa na kosakosa kadhaa ikiwemo za mapema kutoka kwa Shomari Kapombe na Prince Dube.

Bao pekee katika mchezo huo lilifungwa na Maxi Nzengeli dakika ya 44 ya mchezo kwa shuti kali akimalizia pasi nzuri ya kugongeana baina ya Prince Dube na Pacome Zouzoua.

banner

Kipindi cha pili mchezo uliendelea kuwa na kasi lakini Simba sc walikosa ubunifu mbele ya lango licha ya kusaidiwa na kasi ya Joshua Mutale.

Mwamuzi Henry Sasii na wasaidizi wake waliingia matatani kwa kukataa penati za Azizi Ki na Kelvin Kijiri huku pia wakikataa bao la wazi la Azizi ki wakisema kuwa alikua ameotea.

Yanga sc sasa itakutana na Azam Fc katika mchezo wa fainali siku ya Jumapili katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited