Home Soka Chama,Inonga Matatani Simba sc

Chama,Inonga Matatani Simba sc

by Sports Leo
0 comments

Wachezaji watano wa Simba Sc akiwemo Henock Inonga, Cloutos Chama, na Shomary Kapombe wamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi dhidi yao baada ya kufungwa na Yanga SC mabao 5-1 siku ya jumapili.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka chanzo cha ndani ya klabu hiyo ni kwamba wachezaji hao tayari wamejulishwa kuhusu hilo huku ikibainika kwamba suala hilo linaweza kutangazwa ama kutotangazwa kwa umma lakini utekelezaji wake unaanza mara moja.

Simba sc ilikubali kipigo hicho siku ya jumapili novemba 5 huku mastaa hao wakiwa uwanjani ambapo wanatuhumiwa na uongozi kutokana na kuonyesha viwango duni kiasi cha kuruhusu mabao hayo.

banner

Chanzo cha uhakika kutoka Simba SC kimesema kuwa uongozi umeshapata ushahidi wa awali kuhusu tuhuma dhidi ya wachezaji hao na sasa imeanza uchunguzi wa kina ili kujiridhisha kuhusu tuhuma hizo ambapo kipindi chote cha uchunguzi mastaa hao watakua nje ya kambi ya timu hiyo.

Kipigo hicho cha mabao 5-1 kutoka kwa mahasimu wao wakuu Yanga sc kimezua kizaazaa klabuni hapo ambapo tayari kocha Roberto Oliveira na kocha wa viungo wametimuliwa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited