Timu ya Simba sc kupitia kwa Afisa Habari wa klabu hiyo Haji Manara imetangaza viingilio vya mechi hiyo ya kimataifa dhidi ya Ud songo ya Msumbiji mchezo utajaofanyika siku ya jumapili uwanja wa taifa.
Mechi hiyo ya marudiano baada ya awali kutoka suluhu nchini Msumbiji kiingilio cha chini kitakua ni shilingi elfu 5 tu huku viingilio vingine vikiwa 15000 kwa Vip B na C huku Platnum itakua 100000 na Platnum plus ikiwa ni 150000.
Pia Manara alisisitiza mashabiki kujaa uwanjani kama ilivyo kawaida ya mechi za kimataifa ili kuisapoti timu hiyo kupata ushindi.