Taarifa kutoka ndani ya Klabu hiyo ni kwamba tayari uongozi wa Simba Sc umemalizana na Beki ya kati kutoka Coastal Union Lameck Lawi baada ya kupeleka kitita cha milioni 205 ambapo Lawi amesaini mkataba wa miaka miwili ndani ya Simba kwa makubaliano ya pande mbili.
Beki huyo bora chipukizi wa ligi kuu msimu uliopita amekua na kiwango kizuri kiasi cha kuzivutia klabu kubwa hapa nchini ambapo licha ya kuwa na ofa kutoka timu zingine lakini Simba sc imefanikiwa kumsajili baada ya kukubaliana dau na Coastal Union ambapo alikua na mkataba wa mwaka mmoja umesalia.
Tayari mchezaji huyo ameshasaini mkataba huo na sasa anachosubiri ni utambulisho pekee hasa pindi ligi kuu itakapomalizika na dirisha la usajili kufunguliwa.
🎯 Usipitwe!
Kuwa wa kwanza kupata habari za moto za michezo nchini Tanzania na duniani kwa ujumla, moja kwa moja kwenye barua pepe yako kutoka SportsLeo Bongo!
- ✅ Matokeo ya mechi
- ✅ Uchambuzi wa kina
- ✅ Habari za ndanii ya timu zako pendwa
✉️ Quality content, no spam. Unsubscribe anytime.
Lawi ambaye ni mrefu anakuja wakati muafaka ambapo mabeki wa kati ya Simba sc Hussein Kazi na Kennedy Juma wamekua na mwenendo wa kusuasua hasa anapokosekana Henock Inonga ambaye dalili zinaonyesha anaweza kuachana na klabu hiyo mwishoni mwa msimu huu.