Home Soka Molinga Kutua Morocco

Molinga Kutua Morocco

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa Yanga sc David Molinga atajiunga na klabu ya RS Berkane inayoshiriki Ligi Kuu nchini Moro mara tu mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu huu.

Kwa mujibu wa Taarifa za ndani Kocha wa zamani wa Yanga Mwinyi Zahera, anatajwa kuwa nyuma ya uhamisho wa straika huyo wa kimataifa wa Congo na ikumbukwe ndiye aliyemsaini klabuni hapo kabla ya kutimuliwa.
“Kila kitu kuhusu uhamisho tayari kimekwisha fanyika na sasa tunasubiri ni mkataba wake na Yanga kumalizika,” Zahera akizungumza na Gazeti la MwanaSpoti.

Licha ya kupigiwa kelele kuhusu kiwango chake na mashabiki wa klabu yake Hadi sasa msimu huu David Molinga ndio kinara wa mabao katika klabu ya Yanga, ameweka kambani mabao 10 kwenye Ligi ya VPL.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited