Home Soka Straika Mkongo Awahenyesha Simba,Yanga

Straika Mkongo Awahenyesha Simba,Yanga

by Sports Leo
0 comments

Straika wa klabu ya Fc Lupopo ya nchini Congo Mpiana Mozizi anazihenyesha klabu za Simba na Yanga ambazo zinachuana vikali kumuwania staa huyo mkali wa nyavu.

Mozizi mwenye mabao 11 mpaka sasa katika ligi kuu nchini Kongo akiwa nyuma ya Jackson Muleka wa Tp mazembe mwenye mabao 12 anawaniwa na klabu hizo huku Simba sc wakiwa wa kwanza kuwasiliana nae huku Yanga nao wakipeleka jina kwa bosi wa Gsm ili kuanza harakati za usajili.

Hata hivyo klabu hizo inabidi zijipange kwani mchezaji huyo bado ana mkataba na klabu yake hivyo itahitajika dau kumng’oa.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited