Home Soka Watatu Simba sc Kuikosa Namungo Fc

Watatu Simba sc Kuikosa Namungo Fc

by Sports Leo
0 comments

Meneja wa Idara ya Habari na Mawasiliano wa Simba SC Ahmed Ally kuelekea mchezo wa Simba wa Ligi Kuu dhidi yq Namungo FC ametaja wachezaji ambao watakosekana katika mchezo huo.

Wachezaji hao ni Sadio Kanoute, Kibu Dennis na beki wao Israel Patrick Mwenda ambao ni majeruhi ambapo Kanoute na Kibu waliumia katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Yanga sc uliofanyika katika uwanja wa Benjamini Mkapa Dar es salaam siku ya Jumapili Novemba 5.

Simba sc inaelekea katika mchezo huo ikiwa na hasira ya kupoteza kwa mabao 5-1 dhidi ya Yanga sc katika mchezo uliopita huku tayari ikiwa imeachana na kocha wake mkuu Roberto Oliveira na timu sasa ipo kwa kocha Dani Cadena ambaye amekaimu akisaidiwa na Seleman Matola.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited