Home Soka Yanga sc Watua Arusha Kibabe

Yanga sc Watua Arusha Kibabe

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha mabingwa wa Ligi Kuu Bara 2023/2024, Yanga kimewasili jijini Arusha leo na kitacheza mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Shirikisho (FA) dhidi ya Ihefu Mei 19, 2024 kwenye uwanja wa Sheikh Amri Abeid Kaluta, kuanzia saa 9:30 Alasiri.

Katika msafara wa klabu hiyo mastaa kama Khalid Aucho,Kennedy Musonda na wengine walionekana wakishuka katika ndege akiwemo Augustine Okrah ambaye hakucheza michezo kadhaa kutokana na kusumbuliwa na majeraha.

Yanga sc inatarajiwa kukutana na upinzani mkali mbele ya Ihefu Fc yenye mastaa wa maana wa kimataifa huku pia ikiwa na kiu ya kutwaa taji la kwanza kubwa nchini tangu ianzishwe ili ipate nafasi ya kushiriki michuano ya kimataifa mwakani.

banner

Mara kadhaa Yanga sc imekua ikipoteza michezo ya ugenini dhidi ya klabu hiyo japo mara ya mwisho iliiadhibu kwa mabao 5-1 katika mchezo wa ligi kuu katika uwanja wa Chamazi jijini Dar es salam.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited