Home Soka Zahera Aipa Ushindi Yanga

Zahera Aipa Ushindi Yanga

by Sports Leo
0 comments

Kocha wa zamani wa klabu ya Yanga sc Mwinyi Zahera ameipa ushindi klabu ya Yanga sc katika mchezo wa jumapili wa hatua ya nusu fainali ya kombe la shirikisho ambao utazikutanisha Simba na Yanga.

Zahera anayeishi nchini kwa sasa alisema hayo wakati akihojiwa na gazeti la championi ambapo alisema kuwa “Yanga wana nafasi kubwa ya kushinda mchezo huo wa nusu fainali kwa sababu kiufundi wamekuwa na hamasa kubwa ya kushinda katika mechi dhidi ya Simba, sasa wanachotaka ni kuendeleza pale walipoishia, japokuwa watu wanasema Simba watashinda ila kwangu mimi ni tofauti.

“Unajua ukiachana na wachezaji wa Yanga lakini uongozi wa GSM wanajua kuandaa timu vizuri katika mechi na Simba sasa lazima wahakikishe wanapata matokeo kwa kuwa ndiyo njia pekee ya wao kupata nafasi ya kucheza fainali, ikiwezekana ubingwa wa kwenda kimataifa, hivyo naamini Yanga watashinda bila tatizo mchezo huo.

banner

“Simba tayari ni bingwa kwa sasa hana cha kupoteza tofauti na Yanga ambao wanahitaji zaidi ushindi hivyo utakuwa ni mchezo mzuri na wenye ushindani mkubwa,” amesema.

Mshindi katika mchezo huo atakutana na mshindi kati ya Namungo na Sahale all Stars kuwania tiketi ya kushiriki michuano ya kimataifa.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited