Home Soka Zahera Atua,Kuwaona Balinya,Sibomana Moro

Zahera Atua,Kuwaona Balinya,Sibomana Moro

by Sports Leo
0 comments

Hatimaye kocha mkuu wa Yanga sc Mwinyi Zahera ametua nchini leo alfajiri akitokea nchini Ufaransa alipokua na mapumziko baada ya kutoka katika michuano ya Afcon na timu ya taifa ya Kongo.

Zahera ametua nchini saa 12 na dakika 4 asubuhi ya leo kwa ndege ya shirika la Rwanda(Rwanda Air) na moja kwa moja ataunganisha kambini Morogoro kuungana na timu iliyopo kambini na atashuhudia mchezo wa kirafiki dhidi ya timu ya Eagle Noir ya nchini Burundi mchezo utakaochezwa katika chuo cha biblia mkoani humo.

Zahera alipewa likizo ya wiki mbili kuanzia tarehe 13 mwezi wa saba nakurejea kwake kumezima tetesi zilizosambaa za kuwa amegoma kushinikiza kulipwa madai yake ya fedha kitu ambacho kocha huyo alikanusha.

banner

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited