Home Soka Mkude,Mo Nov 27

Mkude,Mo Nov 27

by Sports Leo
0 comments

Mahakama Kuu ya Tanzania masjala ya Dar es Salaam inatarajia kusikiliza usuluhishi katika kesi ya kiungo nyota wa Yanga Sc Jonas Mkude ambaye anaidai kampuni ya Mohamed Enterprises (Tanzania) Limited fidia ya Sh 1 bilioni kwa kutumia picha yake katika matangazo ya biashara ya bidhaa zake bila ruhusa yake.

Kesi hiyo ya madai namba 192 ya mwaka 2023ambayo ipo mbele ya Jaji Butamo Philip wa mahakama ambapo ilifika siku ya jana (Jumatatu), Novemba 20, 2023 kwa ajili ya kutajwa ambapo imepangwa kusikilizwa usuluhishi Novemba 27, 2023.

Mbali ya kudai fidia hiyo Mkude ameiomba mahakama hiyo iamuru kampuni hiyo kumlipa mrabaha unaotokana na manufaa ambayo kampuni hiyo imeipata.

banner

Katika madai hayo Mkude aliilalamikia kampuni hiyo kutumia picha yake kutangaza biasha-ra ya huduma zake na bidhaa kupitia mitandao ya kijamii ya Instagram,Facebook na Twitter ikijulikana kama X bila ya kupata ridhaa kutoka kwake.

Mkude alijiunga na Yanga sc akitokea Simba sc ambapo julai mwaka huu klabu hiyo ilitangaza rasmi kuachana na kiungo huyo aliyedumu klabuni hapo kwa zaidi ya miaka 10.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited