Home Soka Simba Sc Yazoa Alama Tatu Jioni

Simba Sc Yazoa Alama Tatu Jioni

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Simba sc imefanikiwa kuchukua alama tatu baada ya kupata ushindi wa 1-0 dhidi ya Geita Gold Sc katika mchezo wa ligi kuu nchini uliofanyika katika uwanja wa Ccm Kirumba jijini Mwanza.

Kocha Dennis Kitambi alifanya utafiti wa kutosha kuhusu mbinu za Kocha Abdelhack Benchika kiasi cha kufanikiwa kuziba mianya yote huku akiwazuia vizuri viungo wa Simba sc wakiongozwa na Fabrice Ngoma na Mzamiru Yassin ambao hawakupata nafasi ya kutoa pasi za mwisho kwa Pa Omar Jobe.

Kocha Benchika alifanya mabadiliko kadhaa ambayo yalizaa matunda hasa baada ya kuingia Luis Miquisone na Babacar Sarr ambao walitengeneza bao la pekee katika mchezo huo baada ya Miqquisone kupiga pasi ndefu na Kibu Dennis kumtengea Sarr dakika ya 82 ambaye alifunga bao lbaada ya mpira kumshinda  kipa wa Geita Gold Fc Costantine ambaye alifanya kazi kubwa tangu mwanzo wa mchezo.

banner

Simba sc sasa imecheza jumla ya michezo 14 ikiwa na alama 33 katika nafasi ya pili ya msimamo wa ligi kuu huku Yanga sc wakiwa kileleni mwa msimamo na alama 40 katika nafasi ya kwanza baada ya michezo 15 ya ligi kuu.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited