Home Makala Mzize,Ramovic Watwaa Tuzo

Mzize,Ramovic Watwaa Tuzo

by Sports Leo
0 comments

Mshambuliaji wa klabu ya Yanga Sc Clement Mzize amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa ligi kuu kwa mwezi Disemba akiwashinda Prince Dube wa Yanga sc na Feisal Salum wa Azam Fc.

Mzize katika mechi nne alizoichezea Yanga sc amefunga goli nne na kuhusika kwenye magoli matatu ambapo kwa ujumla akiwa amehusika katika magoli saba na kuisaidia klabu yake kupaa kutoka nafasi ya tatu hadi nafasi ya pili kwenye msimamo wa ligi kuu.

Hivyo hivyo kocha mkuu wa Yanga Sc Sead Ramovic, amechaguliwa kuwa kocha bora wa Ligi Kuu kwa mwezi Desemba ambapo amewashinda Kocha Rachis Taoussi wa Azam Fc na Fadlu Davis wa Simba sc, alioingia nao fainali.

banner

Ramovic katika michezo minne aliiongoza Yanga sc katika michezo minne na kupata ushindi katika michezo yote huku akifunga magoli 16 na kufungwa mawili.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited