Home Makala Mzamiru Kuikosa Yanga Sc

Mzamiru Kuikosa Yanga Sc

by Sports Leo
0 comments

Kiungo wa klabu ya Simba Sc Mzamiru Yassin anatarajiwa kuwa nje ya uwanja kwa takribani wiki mbili ili kujitibu majeraha yake ya kisigino yanayomsumbua.

Mzamiru aliumia katika mazoezi ya klabu hiyo na hivyo kumfanya awe chini ya jopo la madaktari wa klabu hiyo.

Kutokana na majeraha hayo mchezaji huyo anatarajiwa kuikosa mechi baina ya klabu yake na Coastal Union itakayofanyika machi mosi mkoani Arusha pamoja na ile ya machi 8 2025 dhidi ya Yanga sc itakayofanyika katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

banner

Mchezo huo unaotarajiwa kutoa hatma ya ubingwa wa ligi kuu ya Nbc nchini kwa kawaida huvutia mastaa wengi kutaka kucheza ili kuonyesha uwezo wao pamoja na kupata mgao mkubwa wa fedha mbalimbali ambazo hutolewa kama bonansi kwa mastaa wa klabu hizo.

Hata hivyo pamoja na majeraha bado hata akiwa fiti Mzamiru amekua hachezi mara kwa mara klabuni hapo baada ya kusajiliwa kwa Deborah Fernández na Yusuph Kagoma ambao hucheza pamoja na Fabrice Ngoma katika eneo la kiungo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited