Home Makala Letaaa Mzunguuuu

Letaaa Mzunguuuu

by Sports Leo
0 comments

Mzungu wa klabu ya Simba sc Dejan Georgijević amefanikiwa kufunga bao lake la kwanza kwenye ligi kuu msimu huu katika mchezo wa ligi kuu dhidi ya Kagera Sugar na kuipa alama tatu klabu yake katika ushindi wa mabao 2-0 mchezo uliofanyika katika uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salaam.

Simba sc iliandika bao la kwanza dakika ya 42 kupitia kwa Moses Phiri aliyeunganisha kwa kichwa mpira uliogonga mwamba wa Cletous Chama ambaye alipiga faulo kali iliyomshinda golikipa wa timu ya Kagera Sugar.

Kipindi cha pili kocha Zoran Maki alimwingiza Dejan Georgijević kucheza kama mshambuliaji wa kati hivyo kupelekea kupata bao la pili dakika ya 81 ya mchezo akimalizia mpira uliotemwa na kipa wa Kagera Sugar ambaye alijichanganya wakagongana na beki wake.

banner

Mashabiki wa klabu ya Simba sc waliimba jina la mzungu huyo baada ya dakika 90 za mchezo huku Simba sc ikikaa kileleni mwa msimamo na alama 6 na mabao matano.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited