Home Makala Pamba Jiji Yasajili Dirisha Dogo

Pamba Jiji Yasajili Dirisha Dogo

by Sports Leo
0 comments

Klabu ya Pamba Jiji Fc imekamilisha usajili wa wachezaji wawili kwa mkopo kutoka Singida Black Stars ambao ni Habib Kyombo na Hamad Majimengi ili kujiweka sawa na kurejesha makali yake katika ligi kuu ya Nbc nchini.

Pamba Jiji ambayo inanolewa na kocha Fred Felix Minziro ipo katika hatari ya kushuka daraja endapo haitafanya vizuri katika duru la pili la ligi kuu ya Nbc nchini ikiwa katika nafasi ya 13 ya msimamo ikiwa na alama 11 katika michezo 13 ya ligi kuu.

Wachezaji hao wanatarajiwa kuja kuongeza kasi hasa eneo la ushambuliaji lililoongozwa na George Mpole.

banner

Wachezaji hao wametolewa kwa mkopo mpaka mwishoni mwa msimu huu wa ligi kuu ambapo ndipo watarejea Singida Black Stars ili kulinda viwango vyao kutokana na kutopata nafasi ya kucheza kikosini humo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited