Nyota wa zamani wa Simba,Zana Coulibary amevunja mkataba na mabosi wake wa AS Vita ya Congo.
Zana alikipiga ndani ya Simba iliyotinga hatua ya robo fainali ya ligi ya mabingwa Afrika msimu wa 2018/19 na aliibukia AS Vita ambako waliona uwezo wake alipomenayana nao kwenye mechi hizo za kimataifa.
Habari zinaeleza kuwa hesabu za nyota huyo ni kurejea bongo tena kukipiga upya na timu anazozitaka msimu huu ni Azam Fc na Yanga ili azidi kujipima zaidi uwezo wake.