Home Soka Serikali Yapiga Stop Mashabiki Viwanjani

Serikali Yapiga Stop Mashabiki Viwanjani

by Sports Leo
0 comments

Serikali imepiga marufuku mashabiki wa soka katika mikoa nje ya Dar es Salaam, kuingia viwanjani kutazama mechi za Ligi Kuu zitakazohusisha timu za Simba na Yanga kuanzia leo (Jana) hadi pale itakapojiridhisha .

Agizo hilo limetolewa na Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo kufuatia kukiukwa kwa miongozo iliyowekwa ya kukabiliana na virusi vya Corona vinavyosababisha ugonjwa wa Covid-19 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara uliofanyika juzi katika Uwanja wa Sokoine Mbeya, baina ya Mbeya City na Simba .

Katika taarifa yake iliyotolewa jana jioni, serikali imesema imechukua hatua hiyo baada ya kubaini kutofuatwa kwa miongozo iliyowekwa na serikali kwa ajili ya kukabiliana na virusi hivyo .

banner

 

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited