Home Soka Simba Sc Waifuata Mashujaa Kigoma

Simba Sc Waifuata Mashujaa Kigoma

by Sports Leo
0 comments

Kikosi cha timu ya Simba sc kimewasili mkoani Kigoma kuivaa Mashujaa Fc katika mchezo wa ligi kuu nchini utakaofanyika katika uwanja wa Lake Tanganyika siku ya Jumamosi saa kumi jioni.

Msafara wa kikosi hicho ambacho jana kilifanikiwa kufuzu hatua ya 32 bora ya michuano ya kombe la shirikisho nchini uliwasili katika uwanja wa ndege jijini Dar es salaam asubuhi ya leo ambapo sasa mchana tayari kikosi kimewasili salama mkoani humo.

Mastaa mbalimbali wakiwemo Saido Ntibanzokiza,Mohamed Hussein,Aishi Manula walikua ni sehemu ya msafara wa klabu hiyo uliowasili uwanja wa ndege Kigoma.

banner

Mchezo huo utakofanyika jumamosi saa kumi jioni utakua wa ushindani kutokana kila timu kuhitaji alama tatu muhimu huku Simba sc ikiwa katika nafasi ya tatu ya msimamo wa ligi kuu nchini ikiwa na alama 23 katika michezo kumi ya ligi kuu huku Mashujaa ikiwa na alama 9 katika michezo 12 nafasi ya pili kutoka mwishoni mwa msimamo.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited