Home Soka Matampi Ampiku Diarra

Matampi Ampiku Diarra

by Sports Leo
0 comments

Golikipa wa klabu ya Coastal Union Ley Matampi amempiku golikipa wa klabu ya Yanga Djigui Diarra na kuwa kipa mwenye clean sheets nyingi baada ya kufikisha 15 huku Diarra ambaye hakucheza mechi ya leo dhidi ya Tanzania Prisons akibakiwa nazo 14.

Matampi ambaye hakua na mwanzo mzuri alipojiunga na Coastal Union akitokea nchini Congo Dr ambapo baada ya muda alirejea katika kiwango chake huku kocha David Ouma raia wa Kenya akionyesha kumuamini na kumpa nafasi mara kwa mara kikosini humo.

Kipa huyo amempa changamoto Diara ambaye alitwaa tuzo hiyo mara mbili katika misimu miwili iliyopita ambapo kwa msimu huu amecheza jumla ya michezo 21 na kupata cleen sheet 14 huku Matampi akipata 15 katika michezo 24 ya ligi kuu nchini.

banner

Kipa huyo kutokana na kiwango hicho tayari baadhi ya vilabu vimeanza kumvizia kumsajili hususani klabu ya Simba sc ambayo imeonyesha nia ya kumsajili kuchukua nafasi ya Ayoub Lakred ambaye ana mpango wa kutoongeza mkataba katika klabu hiyo baada ya kupata ofa nono katika nchi za kaskazini.

You may also like

Leave a Comment

Sportsleo Bongo ni tovuti ya kwanza na bora zaidi ya michezo nchini Tanzania, ikileta habari kwa Kiswahili, matokeo ya moja kwa moja, tetesi, na taarifa muhimu kuhusu soka, ndondi, riadha na michezo mingine ndani na nje ya Tanzania.

Edtior's Picks

Latest Articles

Sportsleo Bongo Developed and designed by Mediapix Limited